Monday, February 25, 2013

Kulemaa viungo hakuzuii akili kufanya kazi: YOHANA MAGAYI




YOHANA MAGAYI
Naishi katika wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, nina mke na watoto.

Kazi yangu ni ufundi seremala fani niliyoipata katika chuo cha walemavu Yombo Dar es salaam mwaka 1985  - 1986 na pia Milongo Mwanza 1988 – 1989. Pamoja na hayo nilipata mafunzo ya utetezi wa haki za binaadamu kwa watu wenye ulemavu kutoka ICD, kwahyo mimi ni mwanaharakati pia.
Kwa mujibu wa maelezo ya wazazi wangu, nililemaa baada yakuwa nimeanza kutembea nikiwa na umri wa miaka miwili (2). Niliugua polio iliyonipelekea kukaa kwa muda mrefu na baadae kunisababishia ulemavu kwa ujumla.
Nilipata changamoto kubwa katika kuliendea swala zima la kuoa, hata yule niliyekua natarajia kumuoa kabla alishtuka kusikia kua mimi mlemavu nataka kumuoa! Alifikiri kua tutazaa watoto wenye ulemavu pia. Baada ya mimi kupata mtoto wa kwanza mwaka 1988, aliniandikia barua kwamba sasa niko tayari kuolewa na wewe kwakua sikutegemea kama ungekuja kuzaa watoto wazima. Namshukuru sana mke wangu wa sasa kwa uvumilivu tangu 1988 mpaka leo.
Swala la kuoa au kuolewa nichangamoto sana kwa watu wenye ulemavu wapo wengi wanaotamani kupata wenzi wao lakini inashindikana sababu ya ulemavu walionao. Wengine wanapata wenzi lakini jamii zao zinaendelea kulalamika kwa kuona mtu asiyekua mlemavu akiolewa na mlemavu.
Kuna vikwazo vingi katika kupambana na maisha, kwa ujumla mimi ni Mwenyekiti wa kijiji na niligombea na watu wazima wenye viungo vyao vyote, jamii ilinielewa na kunichagua kuwaongoza. Lakini bado napambana na vikwazo vingi kwasababu kuna watu wanajitokeza na kuuliza maswali: ‘Hivi watu wa jamii hii hawana akili kabisa, inawezekanaje watu zaidi ya 5000 mkakubali kuongozwa na mlemavu, hamuoni kwamba huu ni udhaifu mkubwa?’. Wakati mwingine swala la kupata kipato kwa mtu mwenye ulemavu imekua ni changamoto sana. Kwa mfano sisi tunaoishi katika mkoa wa Mara ambapo shughulikubwa ya kipato ni kilimo, kitu ambacho kwa udhaifu wetu hatuwezi. Shughuli ya pili ni Uvuvi ambayo pia ni ngumu kwetu, kwahyo unakuta kupata kipato ni ngumu sana. Nashukuru kwa kazi yangu hii ya Useremala japokua ni ngumu lakini natenda na ninapata mahitaji. Nayashukuru pia mashirika haya ya ICD na mashirika mengine ambayo tunapokutana yanatupa changamoto za namna ya kujitegemea kuliko kutegemea misaada.
Mwanzoni kabisa nilikua na fikra ya ufundi toka mwanzo na ilikua ya jadi kwasababu hata baba zangu walikua wachongaji. Baadae baada ya kuingia shule nilitamani sana kua mhasibu, lakini ndoto hiyo haikufika baada ya kukosa mtu wakuniendeleza katika masomo pamoja na uwezo mkubwa niliokuanao darasani. Kwakweli mzee wangu alipata udhaifu wa kifikra, aligoma kabisa na kusema kwamba wewe hata nikikusomesha hutoweza kwenda kokote. Namlaumu sana kaka yangu ambaye alikua Dar es salaam wakati huo. Nilimwomba anitafutie nafasi ya kurudia mitihani lakini hakuweza kutekeleza hilo. Nilipokwenda Yombo nilitegemea ningepata nafasi ya kusomea uhasibu lakini baada ya kuikosa nikaamua kujiingiza kwenye ufundi kama ndoto yangu ya kwanza ilivokua. Nashukuru kwamba leo hii inanisaidia sana kwakweli. Imenitunza na kunipa mafanikio makubwa, mpaka sasa nina watoto saba (7) na watatu kati yao wamefikia elimu ya sekondari na ninasomesha wengine hakuna mtoto ambaye amenishinda. Nimefikia malengo yangu kwakweli maana namtunza mke wangu nawatunza watoto wangu pia na sijawahi kumpa mtu kunilelea mtoto hata mmoja kati ya hao saba wote.
Naishukuru sana jamii ya kijiji ninamo ishi, mpaka kufikia kunipa hadhi yakuwa mwenyekiti wa kijiji ni jambo la kushukuru sana kwakweli, inamtizamo wa pekee kabisa, kitu ambacho hata Rais hana mtizamo huo. Naishauri jamii kwa ujumla kuwaamini na kuwaheshimu watu wenye ulemavu, kilicholemaa ni baadhi ya viuongo tu, kitu kinachofanya kazi kumudu maisha ya mtu hasa ni akili, kwahyo tunaweza tukiwezeshwa. Jamii itambue kwamba sisi ni moja kati ya jamii inayofanana nao.
Naishauri serikali kupunguza ule udumavu ilionao. Kwa mfano; kuna sheria ya watu wenye ulemavu lakini wameidumaza tu tangu ilipo pitishwa mwaka 2010 mpaka leo haijatungiwa kanuni. Mpaka tunaelekea katika katiba mpya bado sheria ile haifanyi kazi na bado sina imani kama itafanyakazi. Naishauri serikali ihakikishe sheria ile inapata kanuni na kufanya kazi. Pia walemavu wapatiwe nafasi za kujiendeleza. Nashauri pia serikali ivifungue na kuviendeleza vyuo vya watu wenye ulemavu. Kwa mfano chuo cha Milongo Mwanza kimefungwa kasababu ya kukosa walimu wakati serikali ina bajeti.
Nayashauri mashirika yasiyokua ya kiserikali kama ICD, CCBRTna mengine mengi kuongeza juhudi sababu ndio yaliyosababisha watu wenye ulemavu kutambua haki zao. Nayashauri yaendelee kupiga kelele kwakuwa ndiyo yaliyotupatia mwanga, kwakuwa serikali imeweka kabatini sheria na taratibu zote za kumpatia mtu mwenye ulemavu huduma na haki zake.

Kindly Bookmark this Post using your favorite Bookmarking service:
Technorati Digg This Stumble Stumble Facebook Twitter
YOUR ADSENSE CODE GOES HERE

5 comments:

Gerd Ulrich on December 19, 2020 at 2:48 AM said...

Maisha yangu Maajabu yanashangaza ushuhuda, Jinsi nimepata kisanduku chenye nguvu sana ambacho sasa ni pesa yangu mara mbili kutoka mia hadi elfu ya pesa ndani ya masaa 24, na pia jinsi nimerudisha mpenzi wangu wa zamani, sababu kuu niliwasiliana na Dk Lomi kwa msaada mimi kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, basi ananisaidia ni nguvu kubwa ya kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, na ananipenda na ananithamini sasa, basi mimi na Dr Lomi tukawa marafiki, baada ya mazungumzo kadhaa namuuliza ikiwa kuna njia anaweza kuniganga ili nipate pesa, hapo ndipo aliponiambia juu ya sanduku hili la uchawi, akaniambia kuna aina na saizi tofauti ya sanduku, aliniambia aina zote za sanduku, ningeweza kumudu ndogo tu ya sanduku, baada ya maombi muhimu anayofanya kwenye sanduku, ananipeleka kupitia huduma ya kujifungua, aliniambia niweke pesa ndani, niliweka ndani ya sanduku 100 euro baada ya masaa 24 nikagundua ilikuwa elfu 10 euro ndani, na nimekuwa nikitumia sanduku kwa miezi 7 sasa, mimi na mchumba wangu tunaishi maisha bora, ikiwa unahitaji b ack mpenzi wako au pesa spell wasiliana na Dr Lomi kwa barua pepe: lomiultimatetemple@gmail.com au WhatsApp namba +2349034287285 unaweza pia kumwandikia kupitia Jina la Mtumiaji la Snapchat: drlomi20 atakusaidia nje, asante kwa kusoma,

Kwaheri Gerd Ulrich

Anonymous said...

Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe nikiwa nimesimama peke yangu bila mwili kusimama na mimi na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na mchawi huyu wa hodari Dk. ASUBUHI, baada ya kumueleza hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi akiniomba kuwa hatawahi. niache tena, miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa pia una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
*penda uchawi
* kama unataka ex wako nyuma
* Acha talaka
*kuvunja mawazo
* huponya viharusi na magonjwa yote
* uchawi wa ulinzi
*Ugumba na matatizo ya ujauzito
Wasiliana na Dk DAWN kwa barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
Whatsapp: +2349046229159

Anonymous said...

Nilisoma baadhi ya shuhuda kuhusu mtangazaji wa mapenzi anayeitwa DR DAWN kuhusu jinsi ambavyo amesaidia watu wengi kuwarudisha wapenzi wao wa zamani ndani ya masaa 48, kwa dhati nilikuwa nikifikiria kama hiyo ni kweli na ikiwa mwanaume huyu angeweza kusaidia kumrudisha mpenzi wangu ambaye Napenda sana. Niliamua kuwasiliana naye kwa sababu nampenda sana mpenzi wangu na tumetengana kwa miezi kadhaa. Kwa kweli nilimkumbuka sana, nimejaribu njia zingine zote kumrudisha lakini sikuweza. Niliwasiliana na DR DAWN na akaniambia kuwa ex wangu atanirudia baada ya saa 48 zijazo,
Kwa mshangao wangu Ex boyfriend wangu alirudi saa 48 haswa, shukrani kwa Dr DAWN,
Anaweza pia kukusaidia
*Tahajia ili kupata mimba.
*Tahajia ili kuungana tena.
*Tibu ugonjwa wowote.
*tahajia kwa bahati nzuri.
*Tahajia kwa ajili ya mali.
Na wengine.
Wasiliana naye kupitia: dawnacuna314@gmail.com
Whatsapp: +2349046229159

Anonymous said...

Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe cha kusimama peke yangu bila mwili wa kusimama na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na Dk DAWN, baada ya kumwambia. kuhusu hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kiukweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi huku akiniomba kuwa hatoniacha kamwe. tena. Miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
* upendo
inaelezea * inaelezea kivutio
* kama unataka ex wako nyuma
*acha talaka
*kuvunja mawazo
* huponya viharusi na magonjwa yote
* uchawi wa kinga
*Ugumba na matatizo ya ujauzito
* bahati nasibu
* bahati nzuri
Wasiliana na Dk Ediomo kwenye barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
Whatsapp:+2349046229159

Anonymous said...

Habari zenu. Ilikuwa ngumu sana kwangu wakati mpenzi wangu aliniacha kwa mwanamke mwingine. Niliharibiwa kihisia, nilivunjika moyo na sikujua la kufanya ili kumrudisha. Nilihangaika kwa miezi mingi na niliendelea kutafuta msaada kutoka kila mahali hadi nilipopata kujua kuhusu DR DAWN. Niliwasiliana naye na kumweleza shida zangu. Alikuwa tayari kunisaidia na kunisisitiza nifuate taratibu ili aweze kurejesha penzi kati yangu na mtu wangu na pia kuhakikisha tunarudiana wote wawili. Nilipata mahitaji yote na ilifanya kazi hiyo. Baada ya saa 48, nilipata ujumbe kutoka kwa mpenzi wangu akiniuliza tarehe. Sasa tuko pamoja tena na shukrani zote kwa DR DAWN. Anaweza kukusaidia kumrudisha mpenzi wako,
Anaweza kukusaidia na uchawi wa ujauzito,

Anaweza kukusaidia kuponya aina yoyote ya ugonjwa.

ikiwa uko tayari kuamini na kubaki na matumaini. Watumie barua pepe tu kupitia: dawnacuna314@gmail.com
WhatsApp: +2349046229159

Post a Comment

 

| DISABILITY IN TANZANIA INFORMATION PLATFORM © 2012. All Rights Reserved |Designed by MIRAMBO GROUP | Back To Top |