Sunday, April 14, 2013

UBINAFSI WAMKERA MGOSI CHACHA




Naitwa Mgosi Chacha, naishi Musoma mjini katika mtaa wa mkendo. Nina ulemavu wa viungo, kwasasa sijafanikiwa kuwa na familia bado natafuta maisha.

Nilizaliwa nikiwa mzima kama watu wengine, ila baada ya kufikisha umri wa miaka miwili nilipatwa na maradhi ya kienyeji, ambayo kimira yalikua kama miiko kwetu. Baba alikutana na vitu flani ambavyo ni miiko kimira, kwahiyo mi nilipozaliwa ndo nikapatwa na hayo maradhi. Baba na mama walikosa ushirikiano katika swala zima la kuniuguza mimi, hii ilimpelekea mama kunihudumia jinsi anavojua mwenyewe hatimaye ndo nikapata ulemavu.
Changamoto kubwa ninayo kumbananayo ni ubinafsi uliojikita katika jamii. Kwamfano mtu kama mimi nina elimu ya ufundi (welder) na nimesoma chuo kabisa, lakini nikifika ofisini kwa mtu kuomba kazi sipewi kazi. Nakataliwa na kutimuliwa katika mazingira yao, pamoja na kuwaonesha vyeti vyangu kama uthibitisho wa uwezo wangu katika kuifanya kazi hiyo. Nikutokana na hali ya ulemavu nilionao jamii hunichukulia kama mtu asiyeweza kufanya kazi. Na hii ndo ilinipelekea kuamua kujiajiri na kufanya kazi ya kushona viatu.
Naishauri jamii kutuangalia sana sisi watu wenye ulemavu na wasitutenge sababu kulemaa viungo sio kulemaa kila kitu cha mwili wako. Jamii ijitahidi kuwa karibu sana na sisi kwasababu sisi ni kama wao na wao nikama sisi.
Nawashauri watu wenye ulemavu kuondoa ile kasumba ya kutokutaka kujitegemea kwasababu ya ulemavu walionao. Mlemavu anawezakuwa na familia na akategemewa kama watu wengine. Mlemavu sio mtu wa kutegemewa kusaidiwa kwa kila kitu, inabidi kujisaidia wakati mwingine. Ukiwa umelemaa viungo tu na unaakili ya kukuongoza katika mambo mengine kwanini usijitegemee?
Naona kwa wakati huu serikali imeanza kutupa matumaini ya kutukumbuka, hapo awali tulikuwa tumesahaulika kabisa. Nashauri serikali kuziboresha ofisi zake ili ziweze kufikika na watu wa aina zote pasipo kuwabagua watu wenye ulemavu (hususani walemavu wa viungo). Hii itatuondolea ile adha ya kuwaagiza watu wakatuzungumzie haja zetu na badala yake tutaweza kujieleza wenyewe.
Mashirika ya watu binafsi kidogo wana uelewa, hata wakiamua kufanya kitu wanakifanya kwa kuzingatia maoni ya wadau mbalimbali. Nayashauri mashirika na taasisi mbalimbali kushiriki katika kuhakikisha walemavu mbalimbali (ambao wengi wao hawana elimu) wanapatiwa haki zao za msingi.

Kindly Bookmark this Post using your favorite Bookmarking service:
Technorati Digg This Stumble Stumble Facebook Twitter
YOUR ADSENSE CODE GOES HERE

4 comments:

Anonymous said...

Hey there, I'm a new blogger coming from Zandvoort, Netherlands who found you on http://disabilityintanzania.blogspot.com/. Do you have any suggestions for up-and-coming writers? I'm working on beginning my own blog soon but I don't really know where to begin. Do you think I should get started with a free site like Micro Blogs or invest some cash into a pay site? I'm faced with quite a few options and it's all so intimidating... Any tips?

Feel free to surf to my site: sharemyfailure.com

Anonymous said...

I feel like I've seen this page earlier on , but upon spending a while on here it's evident that this is a new
web page. In any case, I'm certainly glad I located it and I'll
add it to my bookmarks to check back often.

my webpage :: http://justinsurancebrokers.com/

Anonymous said...

I stumbled on your blog while I was looking around on http:
//disabilityintanzania.blogspot.com/. Have you got any sort of information on methods to get listed on http://disabilityintanzania.
blogspot.com/? I've really been intending to for quite a while but I never seem to make it happen. Cheers

Feel free to visit my website: moribundo

wanjauchida on March 4, 2022 at 5:21 PM said...

Harrah's Casino Atlantic City - MapyRO
Find all information and best deals 계룡 출장안마 of 거제 출장마사지 Harrah's Casino 구리 출장안마 Atlantic City, New Jersey, Harrah's Atlantic City Address: 3131 평택 출장샵 W. Atlantic City Boulevard, Suite 벳 365 115, Nearby Attractions.

Post a Comment

 

| DISABILITY IN TANZANIA INFORMATION PLATFORM © 2012. All Rights Reserved |Designed by MIRAMBO GROUP | Back To Top |