Sunday, January 13, 2013

CHRISTINA MAUMA




Naitwa Christina Mauma mkazi wa kijiji cha Kiara, nina ulemavu wa macho na sifanyi kazi.

Nina mtoto mmoja ambaye naishinaye na kumtunza. Ulamavu nilionao nilizaliwanao.
Katika maisha ya kila siku nakumbana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukosa msaada wa kumpeleka mtoto shule. Miundombinu kutokua rafiki na ukosefu wa huduma tengamavu kwa watu wenye ulemavu.
Naishauri jamii kuwapenda na kuwathamini watu wenye ulemavu. Watu wenye ulemavu ni sawa na watu wengine wanahitilafu ndogo tu katika viungo vyao ila wanahitaji kupendwa na kuthaminiwa kama watu wengine.
Serikali ijitahidi sana kuwajali na kutekeleza mahitaji ya watu wenye ulemavu kwa vitendo isiishie kuzungumza kwenye majukwaa tu.
Walemavu wenzangu wajitahidi kua karibu na jamii na tusijiweke mbali na hata katika kazi tusaidiane kwa pamoja ili tusiendelee kuonekana kua tuko nyuma sana.
Mashirika na asasi mbalimbali wajitahidi kuzidi kuwatia moyo watu wenye ulemavu bila ubaguzi. Pia mashirika yanapokua yanaita wawakilishi wa kuwasaidia katika shughuli mbalimbali wilayani na mikoani wajitahidi kuwahusisha hata walemavu wasio wafanyakazi. Kitendo cha kuwatumia wafanyakazi pekee kwa mfano; walimu ni kuwanyima walemavu wasio na ajira fursa ya kujifunza na kutetea haki zao.

Kindly Bookmark this Post using your favorite Bookmarking service:
Technorati Digg This Stumble Stumble Facebook Twitter
YOUR ADSENSE CODE GOES HERE

0 comments:

Post a Comment

 

| DISABILITY IN TANZANIA INFORMATION PLATFORM © 2012. All Rights Reserved |Designed by MIRAMBO GROUP | Back To Top |