Thursday, May 9, 2013

ALBINO AFUKUZWA SHULE JIJINI MBEYA KWA MADAI KWAMBA NI MCHAWI

0 comments


Amina Mwamkinga alisema tangu tarehe tisa alipofukuzwa bwenini na wanafunzi wenzie wakitaka aondoke shuleni hapo wakimtuhumu kuwa mchawi majira ya usiku hali iliyomlazimu kuomba hifadhi kwa mlinzi aliyemkubalia na kukesha naye hadi asubuhi  hali iliyopelekea kupigwa na baridi kali kutokana na kukosa nguo za kujisitiri kama Shuka nk.


Hapa Amina akimsimulia mkasa mzima mwandishi wa Mbeya yetu Joseph Mwaisango mara baada ya kupata maelezo yote ya Amina mwandishi alimpigia simu katibu wa chama cha maalbino mkoa wa Mbeya afike ofisi ya Mbeya yetu ili wasaidiane kutatua tatizo hilo.



katibu wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya, Wiliamu Simwale akiwa makini kumsikiliza Amina katika ofisi ya Mbeya yetu


KATIKA Hali isiyokuwa ya Kawaida Uongozi wa Shule ya Sekondari Hollwood iliyoko Mlowo Wilayani Mbozi Mkoa wa Mbeya imemsimamisha shule Mwanafunzi wa kidato cha tatu kwa takribani Miezi Miwili kwa madai kuwa anajihusisha na imani za Kishirikina.
  
Mwanafunzi huyo aliyejulikana kwa jina la Amina Mwankinga(20) ambaye ni mlemavu wa ngozi(Albino) alisimamishwa shule na uongozi wa Shule hiyo tangu Machi 9, Mwaka huu baada ya uongozi wa Shule hiyo kupata taarifa kutoka kwa Wanafunzi wakimtuhumu Mwenzao huyo kuwa ni Mshirikina.
  
Uongozi wa Shule hiyo baada ya kupata taarifa hizo ulimwamuru mhanga wa tukio hilo kuondoka Shuleni hapo pasipo kufuatilia na kujua ukweli wa jambo hilo na kupata udhibiti hivyo kumwacha Mwanafunzi huyo akizurura mitaani asijue hatma ya maisha yake.
  
Mhanga wa tukio hilo Amina Mwankinga alisema tangu tarehe tisa alipofukuzwa bwenini na wanafunzi wenzie wakitaka aondoke shuleni hapo majira ya usiku hali iliyomlazimu kuomba hifadhi kwa mlinzi aliyemkubalia na kukesha naye hadi asubuhi  hali iliyopelekea kupigwa na baridi kali kutokana na kukosa nguo za kujisitiri kama Shuka nk.

Anasema kutokana na hali hiyo Walimu pamoja na uongozi wa Shule hiyo haukuchukua hatua yoyote jambo lililomlazimu kuondoka Shuleni hapo  baada ya kukosa msaada ambapo alirejea Jijini Mbeya anakoishi na Binamu yake.
  
Binti huyo anayesomeshwa na Shirika la Under the SameSun  iliyoko Jijini Dar Es Salaam aliwaambia waandishi wa habari kuhusu mkasa uliompata huku akiomba msaada kwa wasamaria wema kumtafutia Shule ili aendelee na masomo kwa ajili ya kujiandaa na mtihani wa kidato cha nne Mwakani.
  
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya HollyWood Ambukeghe Mtafya, alipopigiwa simu kuhusu tuhumahizo alikiri kulijua suala hilo na kwamba walimrudisha mwanafunzi huyo nyumbani ili kumnusuru na kipigo kutoka kwa wanafunzi wenzie na kuongeza kuwa aliambiwa atafute shule nyingine ili ahamie.
  
Naye katibu wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya, Wiliamu Simwale  alisema alikuwa  halijui suala hilo na kwamba kama lingekuwa suala liko nyeti angejulishwa yeye juu ya hatua zilizofikiwa ambapo Uongozi wa Shule umeendelea kupokea fedha za malipo ya Mwanafunzi pasipo kutoa taarifa kwenye shirika linalolipa.
Mlezi wa Wanafunzi hao kutoka Shirika la Under the Samesun Omary Mfaume amesema kwamba hana taarifa zozote  kuhusiana na tukio hilo na kuongeza kuwa anawasiliana na uongozi wa Shule moja kwa moja ili umweleze juu ya kilichotokea ili taratibu za kumtafutia Shule nyingine zifanyika haraka ili Mwanafunzi aendelee na masomo kama kawaida.

Na Mbeya yetu. 
 

 
Read More ->>

Friday, May 3, 2013

PHOTO OF THE DAY

0 comments

Read More ->>

COME ONE COMA ALL NEVER MISS THIS

0 comments

LETS GET THE COMMUNITY INFORMED ON OUR VALUES AND POTENTIALITIES: Never miss this important EVENT 


Read More ->>

Sunday, April 14, 2013

UBINAFSI WAMKERA MGOSI CHACHA

4 comments


Naitwa Mgosi Chacha, naishi Musoma mjini katika mtaa wa mkendo. Nina ulemavu wa viungo, kwasasa sijafanikiwa kuwa na familia bado natafuta maisha.

Nilizaliwa nikiwa mzima kama watu wengine, ila baada ya kufikisha umri wa miaka miwili nilipatwa na maradhi ya kienyeji, ambayo kimira yalikua kama miiko kwetu. Baba alikutana na vitu flani ambavyo ni miiko kimira, kwahiyo mi nilipozaliwa ndo nikapatwa na hayo maradhi. Baba na mama walikosa ushirikiano katika swala zima la kuniuguza mimi, hii ilimpelekea mama kunihudumia jinsi anavojua mwenyewe hatimaye ndo nikapata ulemavu.
Changamoto kubwa ninayo kumbananayo ni ubinafsi uliojikita katika jamii. Kwamfano mtu kama mimi nina elimu ya ufundi (welder) na nimesoma chuo kabisa, lakini nikifika ofisini kwa mtu kuomba kazi sipewi kazi. Nakataliwa na kutimuliwa katika mazingira yao, pamoja na kuwaonesha vyeti vyangu kama uthibitisho wa uwezo wangu katika kuifanya kazi hiyo. Nikutokana na hali ya ulemavu nilionao jamii hunichukulia kama mtu asiyeweza kufanya kazi. Na hii ndo ilinipelekea kuamua kujiajiri na kufanya kazi ya kushona viatu.
Naishauri jamii kutuangalia sana sisi watu wenye ulemavu na wasitutenge sababu kulemaa viungo sio kulemaa kila kitu cha mwili wako. Jamii ijitahidi kuwa karibu sana na sisi kwasababu sisi ni kama wao na wao nikama sisi.
Nawashauri watu wenye ulemavu kuondoa ile kasumba ya kutokutaka kujitegemea kwasababu ya ulemavu walionao. Mlemavu anawezakuwa na familia na akategemewa kama watu wengine. Mlemavu sio mtu wa kutegemewa kusaidiwa kwa kila kitu, inabidi kujisaidia wakati mwingine. Ukiwa umelemaa viungo tu na unaakili ya kukuongoza katika mambo mengine kwanini usijitegemee?
Naona kwa wakati huu serikali imeanza kutupa matumaini ya kutukumbuka, hapo awali tulikuwa tumesahaulika kabisa. Nashauri serikali kuziboresha ofisi zake ili ziweze kufikika na watu wa aina zote pasipo kuwabagua watu wenye ulemavu (hususani walemavu wa viungo). Hii itatuondolea ile adha ya kuwaagiza watu wakatuzungumzie haja zetu na badala yake tutaweza kujieleza wenyewe.
Mashirika ya watu binafsi kidogo wana uelewa, hata wakiamua kufanya kitu wanakifanya kwa kuzingatia maoni ya wadau mbalimbali. Nayashauri mashirika na taasisi mbalimbali kushiriki katika kuhakikisha walemavu mbalimbali (ambao wengi wao hawana elimu) wanapatiwa haki zao za msingi.
Read More ->>
 

| DISABILITY IN TANZANIA INFORMATION PLATFORM © 2012. All Rights Reserved |Designed by MIRAMBO GROUP | Back To Top |